Proverbs 6:1-5
Maonyo Dhidi Ya Upumbavu
1 aMwanangu, kama umekuwa mdhamini wa jirani yako,
ikiwa umeshika mikono kwa kuweka ahadi
kwa ajili ya mwingine,
2 kama umetegwa na ulichosema,
umenaswa kwa maneno ya kinywa chako,
3 basi fanya hivi mwanangu, ili ujiweke huru,
kwa kuwa umeanguka mikononi mwa jirani yako:
Nenda ukajinyenyekeshe kwake;
msihi jirani yako!
4 bUsiruhusu usingizi machoni pako,
usiruhusu kope zako zisinzie.
5 cJiweke huru, kama swala mkononi mwa mwindaji,
kama ndege kutoka kwenye mtego wa mwindaji.
Copyright information for
SwhKC